Powered By Blogger

Wednesday, January 30, 2019

KIONGOZI NI NANI


KIONGOZI NI NANI
Sehemu  Ya  Kwanza
  Kiongozi:  Ni mtu anayechaguliwa au kuteuliwa na watu ili utekeleza yale yanayotakiwa kutekelezwa.  Au Kiongozi: Ni mtu anayechaguliwa na watu ili kuwa mwaakilishi wao katika Taasisi au Jumuiya ya watu flani.
            Watu wanaweza kuwa viongozi kutokana na sifa au karama aliyojaliwa na Mungu. Kiongozi naweza akawa mtu aliyesomea pia kuna baadhi ya watu wao huzaliwa wakiwa na  karama hiyo ya uongozi, watu hawa wanaweza wakawa viongozi wazuri sana pengine kupita hata wale waliosomea.
            Katika ulimwengu watu kuna aina mbili za viongozi;-
1.         Viongozi wa kuchaguliwa
2.        Viongozi wa kuteuliwa/kurithi

****************
MAJUKUMU  YA  KIONGOZI;-
         i.            Kutekeleza majukumu aliyopewa na watu
       ii.            Kuwaunganisha watu
     iii.            Kusimamia raslimali za watu
      iv.            Kusimamia na kulinda “ukweli”  katika kuleta maendeleo ya watu
Kiongozi akitimiza majukumu hayo atakuwa ni kiongozi mzuri na mwenye kupendwa na watu kwa sababu ya  utumishi wake mzuri kwa watu. Watu wanaweza kutamani na kuonja maisha ya furaha kupitia yeye, na ndivyo ilivyo kwa kiongozi mzuri anayejali na kutekeleza majukumu yake.
UONGOZI  MBAYA;-
             Katika uongozi kuna baadhi ya watu wao hutumia Mamla hayo ya uongozi kufanya ndivyo sivyo kwa sababu ya manufaa yao binafsi. Jambo hili huathili sana watu wanyonge wanaotegemea viongozi wao kufaya kadri ya matakwa na misingi ile uliyompelekea yeye kuchaguliwa au kuteuliwa na watu.  Kiongozi anaweza akawa kikwazo kwa watu kwa sababu ya kutumia nguvu na mamlaka aliyopewa kunyanyasa watu na kuhujumu mali na haki ya binadamu.

            Asilimia kubwa ya watu wanaotarajia kuteuliwa au kuchaguliwa huwa ni wazuri wa kushawishi na huwa wanamvuto flani kabla hawajawa viongozi, hawa hufanya hivyo kwa sababu bado hawajapata uongozi, na huwa ni watu wa watu sana.
           Uongozi vile vile unaweza kumtia mtu ‘ujinga’ au ‘ukatili’ kwa sababu ya mitazamo binafsi. Uongozi  unawafanya viongozi wa Serikali pia Dini, kutumia uongozi huo waliopewa kunyanyasa watu.  Wao hujiona ni bora sana kupita watu wengine, wao hujiona si wakosefu, wao hujiona wapo sawa katika kile wanachokifanya, wao huyaona makosa ya watu wengine kuliko yao, wao hulimbikiza makosa yao kwa vijakazi wao waonekane wazuri, wao huwaona ni watumwa na watu wasiojielewa watumishi wengine. Hizi ni baadhi ya sifa za viongozi wanaotumia mamlaka yao vibaya.

********************************
Inaendelea……………………………..











Mayumba Publisher
Msalala-Kahama, Contact. +2257-6925-3139
Author; John  Christopher

Email.  Johnchristopher220@gmail.com,  Contact; +2257-5509-2885


No comments: